0:00
6:36
6:36

MAGOLI YOTE YA LEO YANGA SC 4-0 JKT TANZANIA, BOKA, BACCA, KANGWANDA NA SHALULILE GOALS

Sports

#Yangasc #Alikamwe #Ligikuu HAWA YANGA WANATISHA HATA KAMA UNA CHANGAMOTO YA KUONA MBALI FULL TIME Yanga SC 4-0 JKT Tanzania 29' ⚽Kangwanda 34'⚽Bacca 🅰️ Zakouani 39' ⚽ Boka 🅰️Kangwanda 64' ⚽ Shalulile 🅰️Kangwanda Imekuwa mechi ya offense VS Defense JKT Tanzania walianza mechi wakiwa wanaonekana Kwa vitendo wakitaka sare ya 0-0 ,walikaa nyuma ya mpira na dakika zote ilikuwa ni wao kumzuia Yanga asipate goli Kwa njia yeyote. Njia hii aliyoichagua Jkt Leo ilihitaji uvumilivu na nidhamu kubwa sana ya mchezo Ili kukabiliana vyema na Yanga. Yanga ya Manqoba inafanya Pressing ya hatari,wakiwa hawana mpira Kasi Yao ni kubwa sana ya kuurejesha mpira kwenye himaya Yao,na wakipata mpira Wana Kasi mno na ndio imewapa Wakati mgumu Jkt Tanzania . Huyu Albert Kangwanda ameshajitambulisha kwenye ligi ya Tanzania kama mchezaji kamili,anafunga ana tengeneza pia super game kwake,Kafunga na kapiga magoli 2 Leo. Goli la pili la Yanga la free kick limetengenezwa Kwa viwango vya juu na hapa inakuja Kuonekana faida ya Yanga kuwa na Kocha maalumu wa Set Pieces,hili goli ni la ufundi mno. Leo JKT Tanzania amekutana na Quality ya juu mno,ukirejea magoli alivyofungwa utagundua huhitaji Kuwalaumu kuanzia Wachezaji na Benchi la ufundi,wametoa walichonacho na wamepokea kinachostahili. Djigui Diarra Leo clean sheet imepatikana kwake.

ADVERTISEMENT
Comments 0 Be the first to comment