#Yangasc #GaboroneUnited #CAF Shirikisho la Soka Afrika (CAF) limefanya droo ya hatua za awali za Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho msimu wa 2026/27, ambapo wawakilishi wa Tanzania wamepata wapinzani wao. Katika Ligi ya Mabingwa Afrika, Simba SC itakutana na Mighty Wanderers ya Malawi katika raundi ya kwanza ya awali, ikianza ugenini kati ya Septemba 4-6, 2026 na kumalizia nyumbani kati ya Septemba 11-13. Yanga SC nayo imepangwa kucheza dhidi ya Gaborone United ya Botswana, huku ikianza ugenini na kumalizia nyumbani katika tarehe hizo. Endapo Yanga SC itafuzu hatua hiyo, itakutana na mshindi kati ya CFFA ya Madagascar na Lijabatho FC ya Lesotho katika raundi ya pili ya awali kuwania nafasi ya kutinga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Kwa upande wa Simba SC, itahitaji kuvuka kikwazo cha Mighty Wanderers ili kuendelea na safari ya kusaka nafasi ya kucheza hatua ya makundi. Katika Kombe la Shirikisho Afrika, Azam FC ambayo imeanzia moja kwa moja raundi ya pili ya awali, itakutana na mshindi wa mchezo kati ya ASAS Djibouti TΓ©lΓ©com ya Djibouti na ZED FC ya Misri. Nayo Singida Black Stars imepangwa kucheza dhidi ya Al Ghazala SC Wau ya Sudan Kusini katika raundi ya kwanza ya awali, ikianza ugenini kati ya Septemba 4-6 na kurudiana nyumbani Septemba 11-13, 2026.
ADVERTISEMENT