Moshi. Mshambuliaji wa Simba SC na Taifa Stars, Selemani Mwalimu, ameshindwa kuzuia hisia zake na kuangua kilio wakati wa hafla ya ufunguzi wa Uwanja wa Mandela uliopo kata ya Pasua mjini Moshi mkoani Kilimanjaro, iliyoandaliwa kuelekea kuanza kwa michuano ya Zuberi Cup 2026. Mwalimu amelia alipokuwa akisimulia maisha magumu aliyopitia kabla ya kufanikiwa katika soka, akisema uwanja huo una kumbukumbu nyingi za safari yake ya kutafuta mafanikio. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Moshi, Mwalimu amesema akiwa pamoja na rafiki yake, Maulid, walikuwa wakifika uwanjani hapo usiku wa manane kufanya mazoezi licha ya kukosa vifaa muhimu, wakiamini siku moja ndoto zao zingetimia. "Huu uwanja una historia kubwa sana kwenye maisha yangu. Mimi na mshikaji wangu Maulid tuliteseka sana hapa. Kuna kipindi tulikuwa tunakuja kufanya mazoezi usiku wa manane tukiwa hatuna hata viatu, tukiamini ipo siku tutatoboa. Kurudi hapa leo nikiwa hivi, siamini macho yangu. Namshukuru Mungu sana," amesema Mwalimu huku akifuta machozi. Kauli yake iliyoambatana na kilio imegusa wengi waliohudhuria hafla hiyo, huku baadhi wakimshangilia na wengine wakionekana kuguswa na simulizi hiyo ya maisha yake.
ADVERTISEMENT
Kama anarudi kuangalia alipo toka atafika mbali sana atachukuwa baraka nyingi
Bomba mbuzi, Pasua umenikumbusha mbali sna mdogo wangu Selle.
Nakubali Sana usi sahau ulipo toka
Mi sipendi uli bwana dhaa nakupenda nakukubali sana mwalimu
Azimio Primary schools, kitambo sana...
Ndo maisha sele gomes
Anafuraha baada ya kupewa mkataba mpya kwahiyo furaha imepitiriza mpaka analia
😅😅😅 ila sele
kunya kunya fc
Huyo mzee wakupasua kuni bwana sele unabidi umalipe fadbila ulitoka nae mbali Sana kicho la mwona I mpaka kakunulia viatu vya tsh60000 tisha sana
Analia Nini sasa